Rehema za Allah رحمة الله

2.31 MB 79 1 Files
albyan
or download free
[free_download_btn]

Description

Rehema za Allah

"Na Mola wako Mwingi wa kusamehe, Mwenye rehema..." (Qur'an 6:147)

Mwenyezi Mungu ni mwenye upendo na huruma kwa viumbe vyake. Baraka zote na wema katika dunia hii na Akhera ni ushahidi wa wazi wa rehema Zake. Hakika, Uislamu unatufundisha kuwa Allah ni mwenye rehema zaidi kwetu kuliko mama zetu wenyewe. Inawezekanaje iwe vinginevyo, wakati baadhi ya majina na sifa za Allah ni pamoja na:

· Mwenye Kupokea Toba

· Mwenye Huruma

· Mwenye Kumpenda

· Mwenye upole

· Mwingi wa Rehema

· mwenye kurehemu

· Chanzo cha Wema

· Mkarimu Zaidi

· Mwenye Kutoa

Majina haya yote yanaonyesha kwamba Allah ana sifa ya rehema, wema, na ukarimu. Yanasadikisha ukubwa na ukamilifu wa rehema Zake, ambazo huwabariki viumbe vyote. Na Allah anaeleza viumbe hivi kwa kusema: "Ewe mwana wa Adam, ukija Kwangu na madhambi nyingi kama mchanga wa dunia nzima , lakini hunishirikishi na kitu, Nitakuletea msamaha mwingi kama mchanga wa dunia nzima."

Mifano ya Rehema na Baraka za Allah

"Basi ni neema gani za Mola wenu mtazikanusha?" (Qur'an 55:13)

Katika maisha, watu hupokea baraka za Allah kwa mfululizo, iwe ni afya njema, kuona, kusikia, chakula, hewa safi, watoto, utajiri, na nyingine nyingi. Wengine hutumia zawadi za Allah za akili na mantiki kutambua baraka hizi za neema , kuelewa kusudi la kuwepo kwao, na hivyo kujisalimisha kwa Allah. Hata hivyo, wengine hawathamini Rehema ya Allah kwa nafsi zao, ijapokuwa Yeye huwapa riziki na kuwahifadhi licha ya uasi wao Kwake. Wanapewa uwezo wa kusonga, furaha, uhuru wa kufikiri na kutenda, licha ya kumkanusha waziwazi. Kuwepo kwao kusingekuwa bila Rehema ya Allah.

Hatimaye, kila mtu ana hiari ya kutambua baraka zake, kuzitumia kwa njia iliyowekwa na Allah (Mola wa wanaadamu), na kumwabudu Yeye peke yake. Hapo chini, tumeonyesha mwanga wa baraka hizo, kwa sababu "Na mkiuhesabu neema za Allah, hamwezi kuzihesabu. Hakika Allah ni Mwenye kusamehe na Mwenye kurehemu." (Qur'an 16:18)

Uongozi Kupitia Maandiko ya Kiungu na Manabii

"Yeye ndiye aliyekuteremshia Kitabu (Qur’an) kwa haki, kithibitishacho kwa yaliyotangulia, na akateremsha Taurati na Injili." (Qur’an 3:3)

Tangu mwanzoni mwa uumbaji, mwanadamu hakuachwa kukabiliana na changamoto za maisha peke yake. Kwa rehema za Allah, mwanadamu alipokea ufunuo kupitia Manabii, walioufikisha na kuufundisha kwa watu wao ili kuwaongoza na kuwalinda. Ufunuo mkamilifu na wa rehema zaidi ulikuwa Qur’an, na Mtume wa mwisho alikuwa Muhammad (rehma na amani za Allah zimshukie).

Qur’an - ufunuo wa mwisho - ulifuta na kubatilisha ufunuo wa awali, na ni rehema na mwongozo wa mwisho kwa wanadamu. Kama vile Allah alivyotuma Mitume huko nyuma, pia alituma kwa wanadamu mfano hai, mkamilifu na wa kiutendaji wa jinsi mafundisho ya Qur’an kuhusu rehema na uadilifu yanavyopaswa kutekelezwa kivitendo katika maisha yetu ya kila siku. Mfano huu ulikuwa ni Mtume Muhammad (rehma na amani za Allah zimshukie) - rehema kwa walimwengu.

"Na hatukukutuma (ewe Muhammad) ila kama rehema kwa walimwengu wote." (Qur’an 21:107)

Ifuatayo ni baadhi ya kauli za Mtume (rehma na amani za Allah zimshukie) zinazoonyesha rehema, huruma, uvumilivu na mafundisho yake mazuri:

· "Huruma haipo katika kitu chochote isipokuwa huongeza uzuri wake, na haiondolewi kutoka kwa chochote isipokuwa hufanya kuwa pungufu."

· "Aliyekamilika zaidi kati ya waumini kwa imani ni bora wao kwa tabia."

· "Si Muislamu mkamilifu anayekula hadi kushiba huku jirani yake ana njaa."

· "Allah hatamrehemu yule ambaye hawaonyeshi huruma kwa wengine."

Tunavyohitaji sana katika nyakati hizi, kama jamii, ni ushauri mzuri kama huu!

Rehema Kwa Viumbe

Uumbaji wa wanadamu na uwezo wao wote ni rehema kubwa yenyewe. Ukweli kwamba tunaweza kuamka kutoka kitandani, kufanya kazi, kula, kucheza na kulala unatufanya tuwe na shukrani.

"Na miongoni mwa rehema yake, aliwafanyieni usiku na mchana ili mpate kupumzika humo na kutafuta fadhila Zake, na ili mpate kushukuru." (Qur’an 28:73)

Mke au mume ni mojawapo ya neema kubwa, njia ya utulivu na mapenzi.

"Na miongoni mwa ishara Zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao, na akaweka kati yenu mapenzi na huruma. Hakika katika hayo kuna ishara kwa watu wanaofikiri." (Qur’an 30:21)

Rehema nyingine ni kwamba alituumba bila dhambi na hatatuhukumu hadi tufikie umri wa utu uzima na kufanya maamuzi. Hii ni tofauti kabisa na dhana ya "Dhambi ya Asili" katika Ukristo.

Msamaha wa madhambi ni mfano mwingine wa Rehema za Allah, kwani Allah anajua kuwa sisi si wakamilifu na tunakosea. Ukweli kwamba waumini hufanya madhambi haimaanishi kuwa tunapaswa kupoteza matumaini ya Rehema za Allah au kwamba Msamaha Wake umeisha.

"Enyi waja wangu mliofanya dhuluma juu ya nafsi zenu! Msikate tamaa na rehema za Allah: Hakika Allah husamehe madhambi yote: Yeye ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu." (Qur’an 39:53)

Hata wanyama hawajatenganishwa na Rehema za Allah. Wamepewa uwezo wa kusikia na kuona, wanapewa riziki na kizazi, na wanapewa baraka nyingine nyingi. Rehema za Allah zinawafikia kiwango ambacho kwa sababu ya sehemu moja ya Rehema Zake iliyotumwa duniani, "...viumbe Vyake wanahuruma kwa kila mmoja, hata farasi humwondolea mguu wake mbali na mtoto wake ili asimkanyage." Muumba Mwenye Rehema anahakikisha kila kiumbe kinahifadhiwa - kutoka samaki katika kina cha bahari, hadi wadudu ardhini, na ndege angani - wote wanaruzukiwa na Allah.

Jinsi ya Kuongeza Rehema za Mwenyezi Mungu Juu Yetu

"Hakika rehema za Mwenyezi Mungu ziko karibu na wanaofanya wema."
(Qur'an 7:56)

Kwa sababu ya rehema za Mwenyezi Mungu, Ameahidi kusamehe na kuwasitiri wale wanaofuata njia sahihi kama inavyotajwa katika aya ifuatayo:

"Na hakika Mimi ni mwingi wa kusamehe kwa anayerejea (kutubu), akaamini (kwamba Mimi ni Mmoja, na asinishirikishe na chochote), na akafanya matendo mema, kisha akaendelea uongofu."
(Qur'an 20:82)

Sehemu ya kuwa na imani sahihi ni kumwamini na kumtii Mtume wa Mwisho, Muhammad (rehma na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie).

Kwa ufupi, watu wanaopata zaidi rehema za Mwenyezi Mungu ni wale wanaotambua neema na fadhila Zake; wanazitumia kwa njia inayompendeza Mwenyezi Mungu; wanatoa mali zao kwa ajili ya sadaka na kuwasaidia wahitaji; wanatumia pesa zao kuwatunza mayatima; wanatumia ulimi wao kuzungumza kwa kusema maneno mema; na wanatekeleza matendo mengine ya heshima yaliyoamriwa na Mwenyezi Mungu.

Mtume Muhammad (rehma na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie) amesema:
"Mwenyezi Mungu atawarehemu wale wanaowaonea huruma watu. Waoneeni huruma wale walioko ardhini - Yule Aliye Mbinguni atakuoneeni huruma."

Hapa chini ni njia za kupata Rehema za Mungu.

"Mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume wake ili mpate rehema." (Qur'an 3:132)

Kwa kufuata mafundisho ya rehema na uadilifu yaliyomo kwenye Qur'an: "Na hiki ni Kitabu Tumekiteremsha kimebarikiwa; basi kifuateni na mjilinde (na uovu), ili mpate rehema." (Qur'an 6:155)

"Simamisheni swala na toeni zaka na mtiini Mtume ili mpate rehema." (Qur'an 24:56)

Kuomba Rehema kwa dhati kutoka kwa Mungu: "Mola wetu! Usiyapotoshe nyoyo zetu baada ya kutuongoza, na utupe rehema kutoka Kwako; hakika Wewe Ndiwe Mtoaji." (Qur'an 3:8)

Rehema na Uwajibikaji

Pamoja na sifa ya rehema ya Mwenyezi Mungu, kuna sifa ya uadilifu.

Mwenyezi Mungu ni Mwenye Rehema zaidi.

"Hakika, kwa Wacha Mungu kuna Bustani za Neema mbele ya Mola wao. Je, tutawafanya Waislamu kuwa kama wakosaji? Kuna nini kwenu? Mnahukumu vipi?" (Qur'an 68:34-36)

Hata hivyo, Yeye pia ni Mwepesi wa Hesabu. Mtu hawezi kujaribu kumdanganya Mwenyezi Mungu na kutumia rehema yake vibaya kwa kuendelea kufanya madhambi zilezile bila toba ya kweli au kuazimia kutorudia kwenye madhambi tena.

"Na toba si yenye kufaa kwa wale wanaoendelea kufanya maovu mpaka mauti inawajia, ndipo aseme: Sasa nimetubu; wala kwa wale wanaokufa hali ni makafiri." (Qur'an 4:18)

Waislamu wanahimizwa kuwa na matumaini ya thawabu kwa matendo mema, huku wakihofia madhambi wanazoweza kufanya. Wanapofanya madhambi, wanatubu kwa kweli, na wanatarajia kusamehewa. Na hatimaye, wanaridhika na maneno ya Muumba wao, na wanayashikilia karibu na mioyo yao:

"Hakika Mwenyezi Mungu ni Mpole sana na Mwingi wa Rehema kwa watu." (Qur'an 22:65)

Similar Downloads

No related download found!